Nimeyatamani kweli machungwa...Niwaambie kitu nilipokuwa mwanafunzi wa darasa la kwanza na pili. Shuleni kwetu Lundo kulikuwa na miti mingi sana ya matunda mbalimbali mojawapo machungwa...Basi nakuambieni baada ya shule unaaga nyumbani kwenda kuchota maji au kuokota kuni kumbe kula machungwa ya shule...shhhh.:-(.....Ila mmhhh ilikuwa ukikamatwa na mlinzi basi ni viboko tu ...Kaaazi kwelikweli:-) PAMOJA DAIIMA NA MWANZO MWEMA WA MWISHO WA JUMA. PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA. Kapulya.
 
Top