
Joyce Korvick Mkurugenzi wa masuala ya usalama wa kitengo cha FDA anasema kwamba, kwa kuwa dawa hizo zinatumiwa sana na watu wengi, ni muhimu kwa watu wote kufahamu madhara yanayoweza kusababishwa na dawa hizo. Maafisa hao pia wamewataka madaktari kuwaandikia tu dawa hizo wagonjwa ambao hali zao ni mbaya mno, na kusisitiza kuwa faida ya dawa hizo pale zinapotumiwa mara chache ni zaidi ya hatari inayozisababisha.
Huko nyuma pia wataalamu walisema kwamba, dawa hizo za kutibu kiungulia zinahusiana na ongezeko la hatari ya maambukizo ya bacteria aina ya C. difficile anayesababisha ugonjwa wa kuharisha.
Dawa hizo ni kama zile za Emsomeprazole, Dexlansoprazole, Lansoprazole, Emprazole/Sodium Bicarbonate, Pantoprazole, Rabeprazole na Rabeprazole.
Ndugu mdau kama wewe ni miongoni mwa wanaotumia dawa hizo, basi jihadhari kabla ya hatari!